Monday, 17 July 2017

WEST HAM UNITED WAJIKITA KWA JOE HART.



KIPA Joe Hart anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya tayari kwa kujiunga na  klabu ya West Ham United kwa mkopo kutoka Manchester City



West Ham walikuwa wakitafuta kipa mpya kipindi hiki cha majira ya kiangazi na wamefanikiwa kumshawishi kipa huyo wa kimataifa wa Uingereza.

Mkataba wa Hart unatarajiwa kumalizika mwaka 2019 katika klabu ya City na inadaiwa kuwa tayari alishaambiwa atafute klabu mpya na meneja Pep Guardiola.

City walimruhusu Hart aende kwa mkopo katika klabu ya Torino msimu uliopita na sasa anatarajiwa kuhamia Uwanja wa London huku Guardiola akiwa tayari kumlipa nusu ya mshahara wake.



No comments:

Post a Comment