Thursday, 6 July 2017

UCHAGUZI CHAMA CHA WATAALAMU WA TIBA ZA MICHEZO



Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya Chama cha Wataalamu wa Tiba za Michezo (TASMA), kimetangaza Uchaguzi Mkuu wa chama hicho kwamba utafanyika Agosti 5, mwaka huu katika Ukumbi wa Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam.



“Wanachama wote wanakaribishwa kushiriki kwa namna moja au nyingine katika zoezi hili muhimu sana,” amesema Mwenyekiti wa kamati hiyo, Leslie Liunda alipokuwa anatangaza ramani ya mchakato wa uchaguzi huo leo Alhamis Julai 06, 2017.

Amesema: Mwanachama ye yote anayependa kukiongoza chama hiki anaombwa kuchukua fomu katika ofisi za Olimpiki Maalumu, zilizoko jirani na Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam kwa ajili ya kugombea nafasi anayoona kuwa anaweza kuimudu.”

Nafasi zinazowaniwa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mweka Hazina ambao fomu zao zinapatikana kwa Sh 200,000 wakati nafasi za wajumbe wa Mkutano Mkuu TFF na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji fomu zao zinapatikana kwa Sh 100,000.

No comments:

Post a Comment