Mustakabali
wa meneja wa Chelsea, Antonio Conte uko mashakani baada ya meneja huyo
kukasirishwa na shughuli nzima ya usajili katika klabu hiyo (Daily Mirror).
Hatua
ya Manchester United kutaka kumsajili Romelu Lukaku, 24, haihusiani na mkataba
ambao utamrejesha Wayne Rooney, 31, Everton (Liverpool Echo).
Chelsea
bado wanatarajiwa kujaribu kumsajili Romelu Lukaku, 24, licha ya taarifa kuwa
mchezaji huyo amekubali kuhamia Manchester United kwa pauni milioni 75 kutoka
Everton (Guardian).
Mshambuliaji
wa Real Madrid Alvaro Morata, 24, ameachwa "kwenye mataa" baada ya
Manchester United kumsajili Romelu Lukaku. Morata alikuwa na uhakika kuwa
anahamia Old Trafford (Independent).
Romelu
Lukaku amekubali kusaini mkataba wa muda mrefu Manchester United na mshahara wa
pauni 250,000 kwa wiki (Daily Star).
Chelsea
huenda wakakabiliwa na tatizo la mshambuliaji baada ya Diego Costa kuanza kuaga
wachezaji wenzake kufuatia kuambiwa na Antonio Conte kuwa hayuko kwenye mipango
yake msimu ujao (Daily Telegraph).
Chelsea
wanajiandaa kutoa dau "kubwa" kumtaka kiungo wa Real Madrid James
Rodriguez (AS).
Chelsea
sasa wameelekeza macho yao kwa mshambuliaji wa Swansea Fernando Llorente, 32,
baada ya kushindwa kumpata kwa mkopo mwezi Januari (Evening Standard).
Haki
miliki ya picha Getty Images Image caption Carles Puyol
Barcelona
wamekasirishwa na nahodha wao wa zamani Carles Puyol, baada ya mchezaji
anayemwakilisha Eric Garcia, 16, kuamua kuhamia Manchester City (Independent).
No comments:
Post a Comment