Friday, 7 July 2017

KIKOSI CHA STARS KITAKACHOSAKA MSHINDI WA TATU COSAFA,



Kikosi cha Taifa Star leo kitashuka dimbani kutupa karata yake ya mwisho kusaka mshindi wa tatu wa kombe la COSAFA dhidi ya Lesotho.



Kocha mkuu wa kikosi hicho Salim Mayanga amefanya mabaliko kwenye kikosi hicho kuelekea kwenye mchezo huo ambao utatoa taswira ya nani awe mshindi wa tatu katika michuano hiyo.

Katika mchezo wale Mayanga amemwanzisha golini Saidi Mohamed namba mbili ni Shomari Kapombe huku namba tatu akicheza Gadiel Michael, nne na tao wanacheza Salim Mbonde na Nurudin Chona, 

Himid Mao yeye atacheza namba sita namba nane ikichezwa na Salmin Hoza kumi ikichzwa na Raphael Daudi, mambinga ni Shiza Kichuya na Simon Msuva, mpachika mabao atacheza Stamil Mbonde.

Kikosi cha leo Mayanga amepanga wachezaji wote wanaocheza ligi ya nyumbani kwa lengo la kujipanga kwaajili ya mchezoo wa CHANI dhidi ya Rwanda Siku ya Jumamosi ijayo kwenye Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

No comments:

Post a Comment