Monday, 3 July 2017

RODRIGUEZ AILILIA MAN U



James Rodriguez  ameamua kwamba Manchester United ndio klabu pekee ambayo angependa kuhamia majira haya ya kiangazi, kwa mujibu wa taarifa kutoka Diario Gol.
 
Nyota huyo wa kimataifa wa Colombia
ambaye msimu uliopita alicheza jumla ya mechi 33 , hakuweza kuingia kwenye kikosi cha jumla cha Zinedine Zidane katika mechi ya fainali ya UEFA.

Amemuambia Rais wa klabu hiyo , Florentino Perez, kwamba atabaki Real Madrid kama hatoruhusiwa kuongea na Manchester United, na hiyo itazidi kumletea Zidane maumivu ya kichwa.

No comments:

Post a Comment