Sunday, 2 July 2017

MAYANGA ADHIHIRISHA VITENDO DHIDI YA MANENO


Kocha Mkuu wa Taifa Stars Salum Shaban Mayanga ameiwezesha Stars kufika hatua ya nusu Fainali ya michuano ya COSAFA inayoendela  Afrika Kusini.


Kocha huyo ambae  amekua akikosolewa sana wa wadau wa mpira
pamoja na mashabiki wa soka Tanzania mara baada ya kutoka sare ya goli 1 kwa 1dhidi ya Lesotho katika mchezo wa kufania kufuzu mataifa huru ya Afrika, lakini jana amewaumbua mashabiki hao ambao wamekua wakimbza.

Zifuatazo ni rekodi ambazo Mayanga amezivunja.

KOCHA Salum Mayanga ameweza kuiendesha Stars kwa mechi 7 bila kupoteza tangu awe kocha mkuu ameshinda 4 na sare  3 na kuvunja rekodi ya Maximo.

Maximo aliweza kuiendesha stars kupata matokeo katika michezo 5 na katika mitano hiyo alishinda 2 na kutoka sare  3 na mchezo wake wa 6 aliangukia pua kwa kipigo cha 4-0 kutoka kwa Senegal ya kina Mamadou Niang.

MAYANGA Rekodi zake:

Tanzania v Botswana =2-0

Tanzania v Burundi =2-1

Tanzania v Lesotho =1-1

Tanzania v Malawi =2-0

Tanzania v Angola =0-0

Tanzania v Mauritius 1-1

Afrika Kusini v Tanzania 0-1

MARCIO MAXIMO :

Tanzania v Burkinafaso = 2-1

Tanzania v Kenya =0-0

Tanzania v Angola 1-1

Tanzania v Msumbiji =0-0

Tanzania v JK Congo
=2-0

Tanzania v Senegal 0-4

Hizo ni Takwimu za Mayanga vs Maximo za michezo yao ya kwanza

Makocha waliomfuata Marcio Maximo ambao ni Jan Poulsen (Denmark),Kim Poulsen (Denmark) ,Mart Nooij (Netherlands) na Boniphace  Mkwasa (Tanzania) hakuna aliyefikia rekodi hizi za kocha Mayanga.


No comments:

Post a Comment