Wanachama na mashabiki wa klabu ya
Simba wameombwa kuendelea kuwa kitu kimoja katika kipindi hiki ambacho
viongozi wao wa ngazi za juu wanakabiliwa na tuhuma za utatatishaji wa fedha.
Rai hiyo kwa wanachama na mashabiki
wa klabu ya Simba imetolewa na mjumbe wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo Said
Tully
ambapo amesema hawana budi kukubaliana na hali halizi inayowakabili
viongozi wao.
Amesema pamoja na kutokuwepo kwa
rais wao Evance Aveva na makamu wake Geoffrey Nyange Kaburu bado shughuli za
klabu ya Simba zitaendelea kufanyika.
Hata hivyo Said Tully amesema suala
la nani atakaimu nafasi za rais na makamu wa rais wa klabu ya SImba bado
litakua sehemu ya kikao cha kamati ya utendajhi kitakachoketi kesho jijini Dar
es salaam, hivyo ameendelea kuwasisitiza mashabiki na wanachama kuwa watulivu.
No comments:
Post a Comment