Wednesday, 5 July 2017

KILA LA KHERI TAIFA STARS.



TIMU ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars leo inashuka katika dimba la Moruleng Kucheza na Zambia katika mchezo wa nusu fainal ya kombe la COSAFA mchezo utakaochezwa saa kumi na mbili kamili kwa saa za afrika mashariki. 



Taifa stars imetinga hatua ya nusu fainali baada ya kumwondosha mwenyeji Afrika ya Kusini kwenye hatua ya Robo fainali kwa ushindi wa bao 1 lililofungwa na Eias Maguli katika kipindi cha kwanza.

Taifa stars ambayo imecheza michezo minne bila kufungwa ambapo imeshinda michezo miwili na kutoka sare michezo miwili  katika mashindano ya COSAFA,  leo inashuka kuwakabili Zambia katika mchezo wa nusu fainali.

No comments:

Post a Comment