Monday, 10 July 2017

KIKOSI CHA TAIFA STARS KILICHOITWA NA KOCHA MAYANGA.



Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Salum Shaban Mayanga ametangaza kikosi kitakachoikabili timu ya taifa ya Rwanda katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za mataifa za mataifa bingwa ya Afrika CHAN utakaochezwa jijini Mwanza mwishoni mwa juma hili.



Mayanga amewaondoa baadhi ya wachezaji aliokwenda nao Afrika kusini kwenye michuano ya ukanda wa Afrika kusini, ambao  wanaokosa sifa ya kushiriki michuano ya CHAN ambayo inatoa fursa kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani pekee.

Mayanga amesema kikosi chake kitaweka kambi kwa siku kadhaa jijini Mwanza kabla ya kucheza na Rwanda, na anaamini muda uliosalia unatosha kukiandaa kikosi chake.

No comments:

Post a Comment