Thursday, 29 August 2013

Udaku wa Soka Leo Alhamisi 29/08/2013

demba ba
demba ba
Meneja wa Newcastle, Alan Pardew ametoa dau la kushangaza kumrudisha Mshambuliaji wa Chelsea ,Demba Ba, 28, ambaye alihama miezi saba iliyopita.

Wayne-Rooney
Wayne-Rooney
Meneja wa Chelsea ,Jose Mourinho anategemea kupunguza machungu yake ya kumkosa Wayne Rooney kwa kumsajili Samuel Eto’o, 32, wa Anzhi Makhachkala na Christian Atsu, 21 wa FC Porto.

etoo
etoo
Mshambuliaji mwenye asili ya Cameroon, Eto’o atatambulishwa kama mchezaji wa  Chelsea siku ya Alhamisi.

mbengue
mbengue
Sunderland wamekutana na ushindani dhidi ya Rennes kumsajili Beki wa Senegal, Cheikh M’Bengue, 25.

Oscar Cardozo
Oscar Cardozo
West Ham wanaweza kumkosa Oscar Cardozo, 30, baada ya Barcelona kuonyesha nia ya kumsajili Mshambuliaji huyo wa Benfica.

javier hernandez
javier hernandez
Meneja wa Tottenham, Andre Villas-Boas anataka kumsajili Mshambuliaji wa Manchester United, Javier Hernandez, 25, lakini wanatakiwa kulipa kiasi cha £15m kumpata Mshambuliaji huyo mwenye asili ya Mexico

guilavogui
guilavogui
Arsenal wako tayari kutoa dau kwa Kiungo wa St Etienne, Josuha Guilavogui, 22, kama watamkosa Yohan Cabaye, 27 ,wa
on Newcastle.
UDAKU WA KIDUNIA  
 Iker Casillas
Iker Casillas
Paris St-Germain wameonyesha nia ya kutaka kumsajili golikipa wa Real Madrid Iker Casillas ,32, ambaye amekuwa akiwekwa benchi tangu ujio wa Carlo Ancelotti ndani ya Bernabeu.

mesut ozil
mesut ozil
Mesut Ozil, 24, ameondoa fununu zote zilizosikika ya kwamba anataka kuhama kwa kusema angependa kuendelea kubaki Real Madrid.Ilisemekana Mjerumani huyo anataka kuondoka sababu ya ujio wa  Gareth Bale, 24.

Burak Yilmaz
Burak Yilmaz
Lazio wako katika majaribio ya kutaka kumsajili Mshambuliaji Mturuki Burak Yilmaz, 28, kutoka Galatasaray.

Dennis Aogo
Dennis Aogo
Klabu kutoka Bundesliga ya Schalke wanakaribia kumsajili Kiungo, Dennis Aogo, 26, kutoka Hamburger SV katika mkataba wa mkopo kwa mwaka mmoja wakiwa na matumaini ya kumsajili baadae.
UDAKU MWINGINE
Lille's French coach Rudi Garcia (R) spe
Mshambuliaji wa Ivory Coast, Gervinho, 26, amekiri ya kwamba amefurahi kuihama Arsenal na amedhamiria kupandisha kiwango chake akiwa klabu yake mpya ya Roma.
Manchester United v Swansea City - Premier League
Mashabiki wa Borussia Dortmund wako kwenye kampeni ya kushinikiza Shinji Kagawa, 24, aondoke Manchester United na kurudi Ujerumani.

No comments:

Post a Comment