Timu ya taifa ya vijana ya Nigeria Golden Eaglets chini ya miaka 17 imetwaa ubingwa wa kombe la dunia kwa vijana.
Kikosi cha cha vijana cha Nigeria kimeweza kutetea ubingwa wake baada ya kutwaa taji hilo la dunia la vijana mwaka 2013 walipoishinda Mexico kwa mabao 3-0.
Mshambuliaji Victor Osimhen ameibuka mfungaji bora kwa kuzipasia nyavu jumla ya mabao 10 katika michuano hiyo.
Afrika ilikuwa tayari imejihakikishia ubingwa wa dunia baada ya mataifa hayo mawili, Nigeria na Mali kufika fainali.
No comments:
Post a Comment