Friday, 30 June 2017

TETESI ZA USAJILI IJUMAA YA LEO.



Barcelona wanamtaka Ander Herera na Riyad Mahrez, kama watashindwa kumsajili Marco Verratti (Sport.es).

Arsenal wamejitoa katika mbio za kumwania nyota wa Monaco Kylian Mbappe, 18, na sasa wataelekeza nguvu zao kumpata Alexandre Lacazette na Thomas Lemar (Mail Online).


Mesut Ozil ameonesha dalili za kubakia Arsenal baada ya kulipia tena chumba maalum cha kutazamia mpira (executive box) ndani ya uwanja wa Emirates (The Sun).

Antonio Conte hajafurahishwa na hatua ya Chelsea kumfuatilia Romelu Lukaku badala ya Andrea Belotti. Conte ameghadhibishwa kwa sababu wachezaji hao wawili bei yao ni moja, takriban pauni milioni 85, lakini mkurugenzi wa ufundi wa Chelsea Michael Emenalo ameamua kumfuatilia Lukaku badala ya Belotti (Daily Star).

Guangzhou Evergrande hawana mpango wowote wa kumuuza Paulinho kwenda Barcelona (Nanfang Daily).
Alvaro Morata amewaambia marafiki wake kuwa ameamua kujiunga na Manchester United na kuwa mkataba tayari "umekamilika" (Daily Express).

No comments:

Post a Comment