Friday, 30 June 2017

Ndoa ya Lionel Messi kufuru.



Mchezaji nyota wa  duniani Lionel Messi amefunga pingu za maisha na mpenzi wake wa tangu utotoni katika mji wake wa kuzaliwa nchini Argentina.

Mchezaji huyo wa Barcelona amerejea katika jiji la Rosario na kufunga ndoa na
Antonella Roccuzzo, ambaye walikutana kabla yake kuhamia Uhispania akiwa na miaka 13.

Wachezaji wenzake Messi, wakiwemo Luis Suárez na Neymar, walikuwa miongoni mwa wageni 260 waliohudhuria sherehe hiyo, kwa mujibu wa tovuti ya BBC SWAHILI.

Katika tukio hilo Maafisa wa polisi wametumwa katika mji huo kudumisha usalama katika hoteli wanamokaa, na kampuni ya kibinafsi ya usalama itadumisha ulinzi ndani kuzuia watu wasioalikwa kuingia.

No comments:

Post a Comment