Wednesday, 18 November 2015

STARS YAFA IKIWA NA MATUMAINI.

TANZANIA imetolewa katika mbio za kugombania tiketi ya kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia za mwaka 2018 zitakazofanyika nchini Urusi, baada ya kufungwa mabao 7-0 usiku huu na wenyeji Algeria katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Mustapha Tchaker mjini Blida.
 
Matokeo hayo, yanaifanya Taifa Stars itolewe kwa jumla ya mabao 9-2, baada ya awali kulazimishwa sare ya 2-2 na Mbweha hao wa Jangwani katika mechi ya kwanza iliyochezwa Jumamosi mjini Dar es Salaam.

kwa mantiki hiyo stars inarudi nyumbani kujipanga upya kwa michuano mingine,
 

No comments:

Post a Comment