Friday, 13 November 2015

ROONEY OUT LEO



Nahodha na mshambuliaji wa timu ya taifa ya England, Wayne Rooney, hiii leo hatoanzishwa kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo, katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki dhidi ya timu ya taifa ya Hispania.

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya England, Roy Hodgson amethibitisha kumuweka pembeni mshambuliaji huyo, kwa lengo la kumpumzisha na kutoa nafasi kwa wachezaji wengine.

Hodgson, amesema tayari ameshazungumza na Rooney juu ya jambo hilo, na wamekubaliana kwa dhati hivyo anatarajia kumtumia mshambuliaji tegemeo wa klabu ya Leicester City, Jamie Vardy, ambaye amemuita kikosini kutokana na umahiri mkubwa anaoendelea kuuonyesha katika ligi ya nchini England.
Amesema maamuzi hayo katu hayawezi kuathiri mfumo atakaoutumia kikosini mwake, kutokana na kuamini kwamba Jamie Vardy, anatosha kuziba pengo la Wayne Rooney ambaye pia ni nahodha wa Man Utd.
Hata hivyo amewahakikishia mashabiki wa soka nchini England na kwingineko duniani kote, kwa kusisitiza kumtumia Rooney katika kikosi chake cha kwanza ambacho kitapambana na timu ya taifa ya Ufaransa kati kati ya juma lijalo.

No comments:

Post a Comment