Tuesday, 10 November 2015

ALICHOKISEMA ROONEY BAADA YA KUMCHAPA MTU KIBAO JANA USIKU.



"Thanks to everyone at WWE for a great night, the kids loved it. Hope you're ok Wade Barrett! Haha………"

Mshambuliaji wa Manchester United Wayne Rooney,Ryan Giggs,Darren Fletcher,Bingwa wa zamani wa WWE John Bradfield Layfield na mtoto wa Wayne Rooney,Kai jana walihudhuria mchezo wa Mieleka,WWE,jijini Manchester.

Katika mchezo huo,mfalme wa WWE,Wade Barrett alianza kumchokonoa Wayne Rooney kwa kusema "katika huu ulingo kuna wanaume wawili ambao wanahadhi ya ubingwa,yeah ni kweli,lakini si Wayne Rooney na Manchester United"
Barrett akawa anamtaka Rooney apande ulingoni na Rooney akasema shuka huku chini, Barrett akaendelea kumchokonoa Rooney akisema " Ninamchukia huyo mwanao (Kai),amekaa hapo akishuhudia baba yake akifeli hahahah ", Rooney akakasirika
Rooney akaamua kusimama na Barrett akamfata pale, ndipo Rooney akampiga kibao kimoja,Barrett akaanguka chini na mashabiki wote uwanjani wakashangilia .
Baada ya pambano hilo kumalizika Barrett alitwit " Kesho ninaenda Old Trafford nataka nikakutane na Rooney huko"
WWE ambao waliandaa tukio hilo kabla walimshukuru Wayne Rooney kwa kukubali kushiriki pambano hilo na kuwafurahisha mashabiki.
Barrett ambaye ni mshabiki wa Klabu ya Preston North End alishawahi kumkosoa Wayne Rooney kwa kujiangusha na kupata Penati na kusababisha timu yake kutolewa na Man United katika kombe la FA mwezi Februari mwaka jana

No comments:

Post a Comment