Wednesday, 7 January 2015

TETESI ZA USAJILI BARANI ULAYA,






KATIKA habari za tetesi za usajili zilizojitokeza hii leo ni pamoja na klabu ya AS Roma wakibakia na matumaini ya kumsajili Petr Cech kutoka Chelsea
pamoja na Jose Mourinho kusisitiza kuwa golikipa huyo hatauzwa katika kipindi hiki cha Januari.

 Kwa upande wa Liverpool wao wamekubali kutoa kitita cha paundi milioni 10 kwa ajili ya kkumsajili nyota wa Bayern Munich Xherdan Shaqiri huku wakiwa na matumaini ya kuzipiga bao Arsenal na Manchester United ambao nao wamekuwa wakimuwinda nyota huyo wa kimataifa wa Uswis.

Klabu ya Arsenal nayo inaripotiwa kutenga kitita cha paundi milioni 64 kwa ajili ya kumuwania Isco kutoka klabu ya Real Madrid. Arsenal wametenga dau hilo hilo litakaloweza kuvunja rekodi ili kuwazidi kete Chelsea, Liverpool na Manchester City ambao nao wamekuwa wakimtolea macho nyota huyo wa kimataifa wa Hispania.

Tukibaki hapohapo Arsenal wanaripotiwa kutupiwa ofa yao ya kumsajili chipukizi wa klabu ya Legia Warsaw Krystian Bielik. Mazungumzo baina ya vilabu hivyo bado yanaendelea huku ikiripotiwa kuwa Legia wanataka kitita cha paundi milioni 2.3 kwa ajili ya kinda huyo.

 Nayo klabu ya Newcastle United imeihabalisha klabu ya Paris Saint-Germain-PSG kuwa hawatamuuza Moussa Sissoko kwa dau la chini ya paundi milioni 25.

 Newcastle wamepania kuendelea kubaki na kiungo huyo hadi mwisho wa msimu huu. Kwa upande mwingine klabu ya West Bromwich Albion imekubali kuwauzia Tottenham Hotspurs mshambuliaji wao Saido Berahino lakini kwa makubaliano ya Spurs nao kuwatoa Aaron Lennon na Andros Townsend.

Inadaiwa kuwa West Brom wako tayari kumuuza mshambuliaji huyo lakini na wao wanahitaji kuimarisha kikosi chao.

No comments:

Post a Comment